Tuesday, October 4, 2016

UPINZANI WAANDAMANA DHIDI YA RAIS KABILA DRC



Upinzani waandamana dhidi ya rais Kabila DRC
  • 19 Septemba 2016

Waandamanaji wameweka vizuizi na kuchoma magari katika mji mkuu wa Kinshasa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo,baada ya maafisa wa polisi kuwazuia kuandamana.

Wanamtaka rais Joseph Kabila ajiuzulu baada ya kukamilika kwa muhula wake mnamo mwezi Disemba tarehe 20 kulingana na mwandishi wa BBC Poly Muzalia.
Chombo cha habari cha reuters kiliwanukuu mashahidi wakisema kuwa maafisa wa polisi walifyatua risasi kuwatawanya waandamanaji.
Upinzani unahofia kwamba bwana Kabila ana mpango wa kuchelewesha uchaguzi wa urais unaotarajiwa mwezi Novemba ili kusalia madarakani.

Maafisa wa uchaguzi na serikali wanasema kuwa uchaguzi huo utaahirishwa kutokana na matatizo ya mipango katika taifa hilo la Afrika ya kati.
Taifa la DRC halijawahi kuwa na ukabidhi wa mamlaka ulio huru tangu uhuru wake zaidi ya miaka 45 iliopita.




Waandamanaji wakiweka vizuizi na kuchoma moto katika barabara za Kinshasa

No comments:

Post a Comment