Tuesday, October 4, 2016

RAIS KABILA AZURU NCHINI TANZANIA




Rais Kabila azuru nchini Tanzania
  • 3 Oktoba 2016

Rais wa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo DRC Joseph Kabila amewasili Dar es Salaam nchini Tanzania kwa ziara ya siku tatu.
Amepokelewa na viongozi mbalimbali wa nchi hiyo akiwemo rais John Magufuli, makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan, Waziri wa mambo ya nje wa Tanzania balozi Augustine Mahiga , Wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama, viongozi mbalimbali wa Serikali, Mabalozi na wananchi.
Image caption Rais Joseph Kabila akiwasili katika katika uwanja wa ndege wa Julius Nyerere nchini Tanzania 

Katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam, Rais Joseph Kabila Kabange amepokea heshima ya kupigiwa mizinga 21 na kukagua gwaride rasmi lililoandaliwa kwa ajili yake na baadaye kushuhudia burudani ya vikundi vya ngoma.
Siku ya Jumanne tarehe 04 Oktoba, 2016 rais Joseph Kabila Kabange atafanya mazungumzo rasmi na mwenyeji wake Rais John Pombe Magufuli, ataweka jiwe la msingi la jengo la mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na baadaye kushiriki dhifa ya kitaifa iliyoandaliwa na mwenyeji wake Rais John Pombe Magufuli, Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Katika ziara yake Rais Kabila anatarajia pia kuzungumzia masuala ya kisiasa nchini mwake ambapo uchaguzi uliopangwa kufanyika Novemba mwaka huu umesogezwa mbele mpaka mwakani jambo ambalo limeleta sintofahamu kwa wananchi wa Kongo.
Kabila ataondoka siku ya Jumatano kurudi Kinshasa.

 Rais Joseph kabila wa DRC akipokewa na mwenyeji wake rais John Pombe Magufuli wa Tanzania alipoanza ziara ya siku tatau nchini humo
 
 BBC   SWAHILI






Upinzani waandamana dhidi ya rais Kabila DRC
  • 19 Septemba 2016
  • Image caption Waandamanaji wakiweka vizuizi na kuchoma moto katika barabara za Kinshasa
Waandamanaji wameweka vizuizi na kuchoma magari katika mji mkuu wa Kinshasa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo,baada ya maafisa wa polisi kuwazuia kuandamana.
Wanamtaka rais Joseph Kabila ajiuzulu baada ya kukamilika kwa muhula wake mnamo mwezi Disemba tarehe 20 kulingana na mwandishi wa BBC Poly Muzalia.
Chombo cha habari cha reuters kiliwanukuu mashahidi wakisema kuwa maafisa wa polisi walifyatua risasi kuwatawanya waandamanaji.
Upinzani unahofia kwamba bwana Kabila ana mpango wa kuchelewesha uchaguzi wa urais unaotarajiwa mwezi Novemba ili kusalia madarakani.
Image copyright AFP Image caption Maandamano DRC
Maafisa wa uchaguzi na serikali wanasema kuwa uchaguzi huo utaahirishwa kutokana na matatizo ya mipango katika taifa hilo la Afrika ya kati.
Taifa la DRC halijawahi kuwa na ukabidhi wa mamlaka ulio huru tangu uhuru wake zaidi ya miaka 45 iliopita.